STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Manchester Utd yaifumua West Brom 3-0

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/73455000/jpg/_73455370_73455369.jpg
Wayne Rooney akifunga bao la pili la Manchester Utd leo
Man Utd defender Phil Jones heads his side into the lead at West Brom
Jones akifunga bao la kwanza la Mashetani Wekundu kwa kichwa

MASHETANI wekundu wakiwa ugenini muda mfupi uliopita imepata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya West Bromwich kiatika mechi ya Ligi Kuu ya England na kuifanya timu hiyo kuiengua Everton kwenye nafasi ya sita ikiifupumua Tottenham Hotspur inayoshuka dimbani baadaye dhidi ya Chelsea.
Mabao ya Phil Jones la dakika ya 34 kwa pasi ya Robin van Persie  lililidu kipindi cha kwanza na mengine ya kipindi cha pili kupitia wa Wayne Rooney dakika ya 65 na Danny Welbeck  kwa pasi ya Rooney dakika ya 82 ilitosha kuifanya Manchester United kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 na kufikisha pointi 48 sawa na Everton, lakini wakitangulia mbele kwa uwiano wa mabo ya kufunga na kufungwa.
Ushindi huo wa ugenini umekuwa afueni kwa kocha David Moyes kuelekea kwenye mbio za kupata nafasi ya ushiriki wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani baada ya mbio za ubingwa kuwa mbali kwao kwa sasa na kuelekea kutemeshwa taji lake.

No comments:

Post a Comment