STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Inter Milan yapigwa nyumbani, Sampdoria yaua Italia

 http://www.iberita.com/wp-content/uploads/2013/04/inter.jpg
MABINGWA wa zamani wa Ulaya, Inter Milan licha ya kucheza nyumbani, imejikuta ikikong'otwa na Atalanta kwa mabao 2-1katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Seria A.
Milan watakuwa wanamuota Giacomo Bonaventura, aliyefunga mabao yote katika kila kipindi na kuipa ushindi timu yake ugenini.
Bonaventura alianza kuwashutua wenyeji kwa kufunga bao la kuongoza katika dakika ya 35 kabla ya Inter Milan kuchomoa dakika moja baadaye kupiyia kwa Mauro Icardi na kwenda mapumziko wakiwa nguvu sawa.
Kipindi cha pili timu zote zilishambuliana kwa zamu na hasa baada ya kufanya mabadiliko ya wachezaji na wageni wakajiandikia bao lao la pili katika dakika ya 90 lililofungwa tena na Bonaventura.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Parma ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 na Genoa, Bologna ikaifumua Cagliari kwenye uwanja wao wa nyumbani na Sampdoria  ikautumia vyema uwanja wake wa nyumbani kwa kuisambaratisha Hellas Verona kwa mabao 5-0 na Udinese ikiwa nyumbani ikapata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sassuolo.
Baadaye watetezi Juventus watakuwa ugenini kuumana na Catania, Napoli itapepetana na Fiorentina na Lazio wataumana na AC Milan ambao msimu huu wamekuwa wakipepesuka katika ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment