STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Kocha Man City atabiri nne zitakazotwaa taji EPL

 http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/05/15/article-2325090-19C218DE000005DC-373_634x413.jpg
MENEJA wa klabu ya Manchester City,  Manuel Pellegrini amesema ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa sasa unaweza kunyakuliwa na timu nne za ligi hiyo.
Pellegrini amesema ukiondoa timu yake na Chelsea inayoongoza msimamo wa ligi hiyo  nyingine zenye nafasi ya kutwaa taji hilo ni Liverpool na Arsenal ambayo jana ilichezea kipigo cha aibu toka kwa Chelsea.
Kocha huyo anayekabiliwa na pambano dhidi ya mahasimu wao wa Manchester, Mashetani Wekundi siku ya Jumanne alisema kwa mwenendo wa Liverpool na hata Arsenal bado zina nafasi licha ya wengi kuzipa nafasi Manchester City au Chelsea kubeba taji hilo msimu huu.
Chelsea inaoongoza msimamo ikiwa na pointi 69 wakati Liverpool inafuatia ikiwa na pointi 65 kisha City yenye pointi sita pungufu dhidi ya vinara hao, ingaw aina michezo mitatu mkononi ikiwa imecheza mechi 28 na Chelsea 3-1.

No comments:

Post a Comment