STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Aston Villa yafa nyumbani yagongwa 4-1 kwa Stoke City

Peter Crouch
Peter Crouch akifunga bao lake dhidi ya Aston Villa
Peter Odemwingie
Peter Odemwingie
TIMU ya soka ya Aston Villa imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufumuliwa mabao 4-1 na Stoke City katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika hivi punde.
Villa ikiyoiduwaza Chelsea wiki iliyopita kwa kuilaza bao 1-0, ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya tano tu ya mchezo kupitia kwa Christian Benteke akimalizia kazi ya Delph.
Hata hivyo wageni walirejesha bao hilo katika dakika ya 22 kupitia Peter Odemwingie aliyemaliza kazi ya mshambuliaji ngongoti, Peter Crouch, ambaye dakika nne baadaye aliipatia Stoke bao la tatu na dakika atatu kabla ya mapumziko N'Zonzi alifunga bao la nne.
Stoke iliongeza bao la nne lililoifanya iiporomoshe Villa katika nafasi ya 10 na kuikalia wao wakibadilishana na wapinzani wao hao wanaowapokea nafasi ya 11 kutokana na kufikisha pointi 37, lilifungwa dakika ya  90 na Cameron.

No comments:

Post a Comment