STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Thomas Mourice arudi nyumbani kujipanga upya kimataifa

Thomas Mourice (wa pili toka kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Bandari Kenya enzi akiichezea klabu hiyo
MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Moro Utd na Yanga, Thomas Mourice amerejea nyumbani baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Bandari-Kenya, huku akisema anafanya mipango ya kuondoka tena kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
Akizungumza na MICHARAZO, Mourice aliyewahi kucheza pia katika Ligi Kuu ya Zanzibar, alisema badala ya kuongeza mkataba na klabu yake ya Bandari inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya ameona ni bora aje nyumbani kupumzika kabla ya kujipanga tena kutoka nje ya nchi.
"Nimerejea hivi karfibuni baada ya kumaliza mkataba na Bandari-Kenya, napumzika kidogo kabla ya kuondoka tena kwenda kucheza soka la kulipwa," alisema Mourice.
Mfumania nyavu huyo mahiri, alisema bado hajawa na uhakika ataelekea wapi safari katika mipango yake ya kucheza soka la kulipwa, lakini alidokeza huenda akaibukia Arabuni au barani Ulaya.
"Mimi kokote naweza kwenda kucheza, lakini katika mipango yangu huenda nikaenda Arabuni au Ulaya kulingana na wakala wangu anayeendelea kunisakia timu wakati napumziko hapa nyumbani," alisema.
Mshambuliaji huyo alijiunga na Bandari misimi mitatu iliyopita pamoja na wachezaji wenzake wa Kitanzania akiwamo Mohammed Banka aliyerejea na kujiunga Asdhanti Utd, Meshack Abel na David Naftal wanaoendelea kucheza mpaka sasa na kuisaidia kumaliza nafasi ya 6 msimu uliopita katika ligi ya nchi hiyo ambayo bingwa wake alikuwa Gor Mahia.

No comments:

Post a Comment