STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Atletico yaibutua Betis, yaiengua Real kileleni kwa muda

Atletico Madrid
Atletico Madrid wakishangilia moja ya mabao yao
IKIWA imesalia kama saa moja na ushei kabla ya mahasimu wa Ligi Kuu ya Hispania, Real Madrid na  Barcelona kupepetana katika pambano lao la El Clasico, Atletico Madrid imekalia uongozi kwa muda baada ya hivi punde kutoka kuifua Real Betis ikiwa kwao kwa mabao 2-0 na kuiengua Real.
Atletico imefikisha pointi 70 sawa na Real Madrid lakini imekwea kileleni kwa uwiano wa mechi baina yao huku uwiano wa mabao Real wakiwa zaidi ya wapinzani wao hao wa jiji moja la Madrid.
Mabvao yaliyozidi kuwapa tumaini la kuwa mabingwa kwa vijana hao wa Diego Simon yaliwekwa kimiani na Gabi katika dakika 58 kwa pasi ya Turan kabla ya Diego Costa kuongeza la pili dakika sita baadaye akimalizia kazi ya Koke.
Katika mchezo huo wenyeji walijikuta wakicheza pungufu baada ya mchezaji wake mmoja Rodriguez kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu katika kipindi cha kwanza.
Hivi sasa uwanjani zipo timu za  Valencia inayoikaribisha Villarreal kabla ya Real Madrid na Barca kuonyesha kazi uwanja wa Santiago Bernabeu ambapo taswira ya ubingwa kwa timu hizo mbili kubwa itafahamika.

No comments:

Post a Comment