STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 23, 2014

Spurs yaizamisha Southampton yaipumulia Arsenal

Christian Eriksen scores Tottenham's second goal
Eriksen akitupia bao lake la pili kimiani dhidi ya Southampton leo
Christian Eriksen
Eriksen akishangilia baada ya kufunga
MSHAMBULIAJI Christian Eriksen leo ameibuka kuwa shujaa wa Tottenham Hotspur baada ya kuhusika na mabao matatu yaliyoizamisha Southampton katika pambano la Ligi Kuu ya England lililochezwa jioni hii.
Mdenish huyo alifunga mabao mawili katika kila kipindi na kutengeneza jingine lililopachikwa wavuni na katika dakika za 'jioni' na Gylfi Sigurdsson na kuipa ushindi murua wa mabao 3-2 Spurs ikiwa kwenye uwnaja wake wa nyumbani.
Eriksen alifunga bao la kwanza katika dakika ya 31 kabla ya kuongeza jingine dakika moja baada ya kuanza kipindi cha pili.
Hata hivyo wageni ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 16 lililofungwa na Jay Rodriguez kabla ya Adam Lallana kuongeza la pili dakika ya 28 na kuwapa wasiwasi wenyeji kwamba huenda wakalala tena nyumbani kama mechi zao kadhaa zilizopita.
Hata hivyo Eriksen alifufua matumaini kwa bao la dakika 31 na kuifanya Spurs kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 2-1.
Kwa ushindi huo Spurs imerejea kwenye nafasi ya tano iliyokuwa imeteremshwa na Everton iliyoishinda Swansea City jana kwa mabao 3-2 kwa kufikisha pointi 56, sita pungufu na ilizonazo mahasimu wao Arsenal waliopo nafasi ya tanoi baada ya jana kukumbana na kipigo cha paka mwizi mbele ya Chelsea.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea muda mfupi baadaye kwa pambano kati ya Astin Villa dhidi ya Stoke City na Jumanne kushuhudia michezoi mingine ukiwamo wa Manchester City dhidi na Manchester United.

No comments:

Post a Comment