STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 22, 2014

Babi azidi kutisha Malaysia atupia mbili kuiokoa UiTM

Babi (kati mbele) ameziodi kudhihirisha ukali wake na kwamba UiTM hawakukosea kumpa unahodha
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Malaysia, Abdi Kassim 'Babi' mwishoni mwa wili aliibeba na kuinusuru timu yake ya UiTM kupata kipigo kwa kutoka nyuma ya mabao 2-0 na kumaliza kwa sare ya 2-2 na Johor katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Malaysia.
Babi alifunga mabao hayo katika dakika ya 70 na 89 na kuifanya timu yake kuambulia pointi moja ugenini iliyochezwa kwenye uwanja wa Pasir Gugand Corporation mjini Pasir Gudang.
Sare hiyo imekuja siku chache baada ya kuisaidia UiTM kupata ushindi wake wa kwanza wa 2-1 dhidi ya Kuala Lumpur SPA baada ya vipigo mfululizo katika ligi ya nchi hiyo.
Mabao hayo mawili yamemfanya Babi aliyeingia mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo kufikisha jumla ya mabao matano tangu ajiunge na UiTM.
Babi ( wa pili kulia) akiwa na wachezaji wenzake wa UiTMya Malaysia

No comments:

Post a Comment