STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 22, 2014

Abou Diaby arejesha tumaini Arsenal

http://www.images99.com/i99/02/36120/36120.jpg
Abou Diaby
BAADA ya kuwa nje ya dimba kwa karibu mwaka mzima, hatimaye Abou Diaby anatarajiwa kuanza kuonekana kwenye kikosi cha Arsenal.
Mchezaji huyo kutoka Ufaransa alikuwa nje ya dimba baada ya kuumia goti Machi mwaka 2013 wakati wa mechi baina yao na Swansea City.
Kwa mujibu wa Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, Diaby 27, amerejea na kungana na wachezaji wenzake kwenye mazoezi ya timu hiyo na huenda akamtumia katika mechi zilizosalia za ligi hiyo.
"Amerejea jumla kwenye mazoezi na sasa ataonekana uwanjani kuitumia timu," Wenger alinukuliwa na mtandao wa klabu hiyo na kuonyesha furaha yake.

No comments:

Post a Comment