STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 22, 2014

Mchezaji gabon afa kwa kikanyagwa kichwani

Sylvain Azougoui enzi za uhai wake
GOLIKIPA wa timu ya AC Bongoville, Sylvain Azougoui amefariki dunia baada ya kukanyagwa kichwani wakati wa mchezo wa ligi huko nchini Gabon. 
Golikipa huyo alifariki wakati akikimbizwa hospitali baada ya tukio hilo wakati wa mechi dhidi ya timu ya Centre Mberi Sportif. 
Azougoui mwenye umri wa miaka 30 raia wa Togo, alikuwa amezuia shuti lililokwenda langoni mwake lakini mshambuliaji aliyepiga shuti hilo alipoteza mwelekeo katika nyasi zilizokuwa zimelowa na kumkanyaga golikipa huyo kichwani. 
Klabu hiyo ilithibitisha habari za kifo cha golikipa huyo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook na kueleza masikitiko yake kwa pengo aliloacha klabuni na kwa familia yake.

No comments:

Post a Comment