STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 22, 2014

Msiba! Mahabusu wa4 askari Magereza wafa ajalini

MAHABUSU wanne na Askari Magereza mmoja wamefariki dunia papo hapo katika ajali iliyotokea eneo la Mkenge, Mkuranga, Pwani.
Taarifa zilizopatikana hivi punde zinasema kuwa dereva wa gari lililokuwa limewabeba marehemu hao yupo hospitalini katika hali mbaya.
Taarifa zinasema kuwa marehemu hao na dereva walikuwa wakitokea Mkuranga kuja jijini Dar es Salaam na kukutwa na ajali hiyo inayopelezwa ni mbaya.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio ni kwamba pick up ya Magereza ilipasuka tairi la kushoto na dereva wake kupoteza muelekeo na kugongana na lori lililokuwa likitokea Kimazichana na gari hilo lililokuwa na mahabusu hao na askari aliyekuwa akiwasindikiza lilipinduka na kusababisha vifo vyao.
Endelea kusoma MICHARAZO MITUPU kupata taarifa kamili, ingawa inaelezwa kuwa majeruhi wamehamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
 

No comments:

Post a Comment