STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 22, 2014

Manchester City yaua 3-1 yaisogelea Chelsea

KLABU ya Manchester City imerejesha tumaini la ubingwa wa Ligi Kuu ya England, baada ya kuilaza mabao 3-1 West Bromwich Albion usiku wa kuamkia leo kwenye pambano lililochezwa kwenye Uwanja wa Etihad.
City ambayo katika pambano lao la mwisho iliponea chupuchupu mbele ya 'vibonde; Sunderland kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2, ilip[ata ushindi huo uliowafanya wafikishe jumla ya pointi 74 baada ya kucheza mechi 34 na inaendelea kushikilia nafasi ya tatu kwenye msimamo nyuma ya Chelsea pointi 75 za mechi 35 na Liverpool pointi 80 za mechi 35.
Ushindi wa City ulianikizwa na mabao Zabaleta aliyefunga dakika ya tatu, Sergio 'kun' Aguero katika dakika ya 10 kabla ya  wageni kupata bao lao la kufutia machozi lililofungwa na Dorrans dakika ya 16 na Demichelis alimalizia kazi kwa kufunga bao la tatu wa wenyeji dakika ya 36.

No comments:

Post a Comment