STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 7, 2014

DC Mkuranga akabidhi nyumba kwa wasanii

Moja ya nyumba walizokabidhiwa wasanii juzi na DC wa Mkuranga Mercy Silla
MKUU wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Silla ameahidi kusaidia kijiji cha wasanii cha Mwanzega wilayani hapa kujengewa barabara, kupata umeme na kuchimbiwa kisima cha maji.
Akizungumza katika sherehe za kukabidhi nyumba 26 za awamu ya pili kwa wasanii wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) iliyofanyika kijijini hapo jana, Mkuu wa wilaya alisema Serikali ya wilaya imeona juhudi za dhati za wasanii kuanzisha kijiji cha kisasa kwa ajili makazi na kilimo hivyo Serikali haiwezi kukaa kimya.
Alisema uwekezaji huo ni mkubwa na kuwataka wasanii kumalizia nyumba zao wahamie na kuahidi kuomba mamlaka husika kukisajili kiwe kijiji chenye uongozi uliokamilika.
Mkuu wa wilaya silla, alishauri SHIWATA kuandika barua Halmashauri ya Wilaya Mkuranga kuomba kupimiwa eneo hilo la makazi lenye hekari 300 ili kupata hati itakayowasaidia kukopa mikopo ya kujiendeleza.
Alimuomba Diwani wa Kata ya Mbezi atumie fursa aliyonayo kuomba Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kufungua barabara ya kwenda kijiji cha wasanii Mwanzega ili ifikike kwa urahisi.
Mkuu huyo pia aliwashauri wasanii hao kuomba Mradi wa Umeme Vijijini (REA)kuingiza umeme kijijini hapo ili kuraahisisha maendeleo ya kijiji hicho nakuahidi kutafuta wawekezaji watakaochimba kisima kirefu.
Alishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni vijana na Michezo kushirikiana na wasanii katika mipango yao ya kujenga nyumba za wasanii.
Mkuu wa Polisi wilaya ya Mkuranga, Thobias Mapalala aliwaahidi wasanii wasitie hofu kuhusu usalama wa mali zao kwa sababu ulinzi unaimarishwa.
Awali Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Cassim Taalib alisema jumla ya nyumba 59 zimekabidhiwa kwa wasanii kati ya 262 wanaochangia ujenzi wa nyumba Mwanzega, Mkuranga.
SHIWATA inamiliki eneo la hekqari 300 kwa ajili ya kujrnga makazi ya waasanii na hekari 500 kwa ajili ya kilimo kwanza wilayani Mkuranga.

No comments:

Post a Comment