STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 7, 2014

Tanzia! Prof Juma Bhalo afariki

ALIYEKUWA gwiji la muziki wa mwambao Afrika Mashariki na Kati Profesa Juma Bhalo, amefariki dunia mwishoni mwa wiki na kuzikwa jana mjini Mombasa.
Mkali huyo wa kuimba, kughani mashairi, alifariki siku ya Jumamosi kwa mujibu kutoka Kenya na kuzikwa jana.
Kwa wanamkumbuka msanii huyo alitamba na nyimbo kadhaa kama Pete, Bunduki Bila Risasi, Alacho Kuku, Ameumbika, Asiyefunzwa na Mamaye, Ganda la Muwa la Jana pamoja na kibao maarufu cha Uliyataka Mwenyewe.
Marehemu alizaliwa mwaka 1942, Malindi na kutamba katika masuala ya muziki miaka ya 1960 akifanya kazi nchini Tanzania na Kenya na alikuja kustaafu miaka michache iliyopita ingawa bado aliendelea kutoa burudani kwa waliomhitaji.
Mungu ilaze roho ya marehemu Juma Bhalo, mahala pema peponi, Ameen

No comments:

Post a Comment