STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 7, 2014

Ridhiwani Kikwete ashinda Chalinze, lakini...?!



Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein akimnyanyua mkono Ridhiwani Kikwete kuashiria ushindi kwa chama hicho.
Habari zilizotufikia zinasema kwamba, mgombea wa CCM, Ridhiwani Kikwete ameibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Chalinze.
Matokeo ya ushindi kwenye Kata zote 15, yanamfanya Ridhiwani bila shaka yoyote kuwa Mbunge mpya wa jimbo hilo.
Hadi tunakwenda mitamboni, Ridhiwani alikuwa akiwatimulia vumbi wapinzani wake kwa kujikusanyia zaidi ya kura 23,612 ambazo ni sawa na zaidi ya asilimia 84.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa CCM kuwabwaga wapinzani wao wakuu, Chadema baada ya Geofrey Mgimwa kushinda kiti cha ubunge Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa katika kipindi kisichozidi mwezi mmoja. Hata hivyo inadaiwa asilimia kubwa ya wapiga kura wameukacha uchaguzi huo kwani waliotarajiwa kupiga kura ni 90,000 kwa maana hiyo ni kama watu 70,000 wamechomoa na hivyo pamoja na Kikwete kushinda, lakini wengi ni kama 'wamemchomolea' kiaina
Kwa taarifa zaidi endelea kuperuzi MICHARAZO. Yafuatayo ni matokeo ya mwisho kwenye baadhi ya vituo vya kupigia kura:-
Talawanda: CCM (1,192), CHADEMA (104), CUF (4).
Msoga: CCM (1,248), CHADEMA (68), CUF (9)
Lugoba: CCM (1,594), CHADEMA (174), CUF (4)
Kiwangwa: CCM (1,180), CHADEMA (80), CUF (14)
Kibindu: CCM (1,131), CHADEMA (300), CUF (3)
Fukayosi: CCM (1,105), CHADEMA (69), CUF (17)
Mandela: CCM (1,394), CHADEMA (112), CUF (8)
Mbwewe: CCM (1,319), CHADEMA (166), CUF (23)
Pera: CCM (1,139), CHADEMA (49), CUF (19)

No comments:

Post a Comment