STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 7, 2014

Shule, Zahanati kufungiwa umeme wa sola bure

Afisa Uhusiano wa Steps Solar Ltd, Moses Mwanyilu (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza mpango wa kampuni yao kufunga vifaa vya kuzalisha umeme wa jua kwa baadhi ya shule, zahanati na vituo vya Polisi.
SHULE  za Sekondari mbili pamoja na Zahanati nne zilizopo Kigamboni, jijini Dar es Salaam zinatarajiwa kufungiwa vifaa vya kuzalisha umeme wa jua bure ili kuwarahisishia watumiaji wa taasisi hizo kuwa na uhakika wa kupata nishati ya umeme kwa saa 24 za kila siku.
Ufungwaji huo pia utahusisha vituo vya kulele yatima, ofisi za serikali pamoja na vituyo vya Polisi na utafanywa na kampuni ya kusambaza vifaa vya umeme wa jua, Steps Solar.
Afisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Moses Mwanyilu aliliambia gazeti hili kuwa, shule zitakazonufaika na mradi huo wanaoufanya Steps na TAREA ni Kidete na Kibugumo, wakati Zahanati ni za Kibugumo, Mji Mwema, Tuangoma na Homboza, huku vituo vya kulelea yatima vitakavyofungiwa vifaa hivyo vya kuzalisha umeme wa jua ni Ungindoni, Mji Mwema , Miti Mirefu na Yatima Charity vyote vilivyopo Kigamboni, wilaya ya Temeke.
Mwanyilu alivitaja pia vituo vya Polisi vya Mjia Mwema na Chanika pamoja na ofisi za serikali za Mji Mwema na Feri navyo pia vitanufaika na mradi huo wenye lengo la kurejesha shukrani zao kwa jamii, sambamba na asasi hizo kuwa na uhakika wa umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma za umeme na hata yale yenye umeme kujihakikisha kuipata nishati hiyo kwa saa 24.
"Kwa kutambua kuwa asilimia kubwa ya watanzania hawapati huduma ya umeme Steps na TAREA tukiwatumia mabalozi wetum Jacob Stephen, Irene Uwoya na Athuman Amri 'King Majuto' tunatarajia kufunga vifaa vya kuzalisha umeme wa jua katika asasa tulizotaja ambazo zitatugharimu kati ya Sh. Mil. 20-30," alisema Mwanyilu.
Aliongeza, kampuni yao ya kuzalisha vifaa vya umeme jua iliasisiwa mwaka jana, na kudai pamoja na kuuza na kusambaza vifaa hivyo alivyoviiuta vya Umeme Nuru, pia wamepania kugawa vifaa na ufungaji bure katika maeneo mbalimbali ya Tanzania hasa yasiyokuwa na uhakika wa umeme, ambayo yataambatana matamasha ya sanaa na elimu pamoja na kugawa zawadi kwa washiriki watakaokuwa wakijibu maswali ya papo kwa papo.
"Lengo ni kutaka kuona mpaka miaka mitano ijayo asilimia kubwa la watanzania wanakuwa wakiwa na uhakiki wa kupata nishati ya umeme na kuwarahisishia shugfhuli zao za kimaendeleo," alisema.

No comments:

Post a Comment