STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 7, 2014

Majambazi yateka magari ya makampuni ya magazeti



Madereva wa gari la magazeti ya kampuni ya The Guardian Rashid Yusuph Kahese (37) kushoto na mwenzake Ally Malinda (44) ambao wamenusurika katika utekaji huo.





Gari la magazeti la kampuni ya The Guardian ambalo limetua Iringa hivi sasa saa 2.40 Asubuhi hii baada ya kupona kutekwa
MAJAMBAZI ambayo idadi yao haikufaanika mara moja usiku wa leo wamefunga barabara ya Morogoro -Iringa eneo la Doma na kufanya unyama wa kutisha kwa wasafiri wa barabara hiyo ikiwa ni pamoja na kuwalazimisha kufanya mapenzi wanaume kwa wanaume na kuwatesa vibaya madereva kabla ya kuwapora mali zao .
Miongoni mwa walioteswa na pamoja na rasta dereva wa gari la magazeti ya kampuni ya globalpublishers ambae anadaiwa kujeruhiwa mkono wake huku dereva wa gari la magazeti ya kampuni ya Mwananchi akinusurika na gari lake kupinduka wakati akikwepa vizuizi vya magogo vilivyotegwa barabarani.
Wakizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com asubuhi ya leo mjini Iringa wahanga wa tukio hilo Ally Malinda (44) mkazi wa Itunda Dar es Salaam na Rashid Yusuph Kahese (37) mkazi wa Mbezi jijini Dar es Salaam ambao kwa pamoja wanaendesha gari ya magazeti ya kampuni ya The
Guardian walisema kuwa tukio hilo lilmetokea mida ya saa 8 usiku wa leo hadi saa 11 Alfajiri baada ya watekaji hao kuachia mateka hao .
Malinda alisema kuwa kabla ya kufika eneo ambalo watekaji hao walikuwa wamewateka abiria wengi zaidi walikutana na makundi ya watu waliotekwa na kuporwa ambao walikuwa wakiwasimamisha wasiendelee na safari ila hawakusimama wakijua ni wezi .
" Tulienda mbele kidogo tukakutana na kundi jingine ila bado tulipuuza na kupita baada ya kufika mbele ndipo tuliona magari yakiwa yamegeuka huku na kule huku wengine wakiteswa na ndipo tulipofanikiwa kugeuza gari letu lenye namba za usajili T 812 CNZ na kukimbia .
Hata hivyo alisema polisi Morogoro walipigiwa simu ila hawakuweza kufika hadi majira ya saa 11 Alfajiri watekaji hao walipoamua kuwaachia mateka.
" Kila tukimpigia kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro aliishia kusema kuna askari wametumwa kuja eneo la tukio ila hadi asubuhi hakuna askari aliyefika .....na majeruhi wamepelekwa Hospital ya mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi"
Mtandao huu wa matukiodaima .com unaendelea kumtafuta kamanda wa polisi wa mkoa wa Morogoro ili kuzungumzia tukio hilo zaidi .
Chanzo: francis godwin blog

No comments:

Post a Comment