STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 1, 2014

Jahazi la Sundrland lazidi kuzama England

Andy Carroll akishangilia bao lake jana
JAHAZI la timu ya Sunderland limezidi kuzama kwenye Ligi Kuu ya England baada ya usiku wa kuamkia leo kubamizwa nyumbani kwao kwa mabao 2-1 na West Ham United katika mechi pekee ya ligi hiyo iliyochezwa Jumatatu.
Mabao ya Andy Carroll la dakika ya 9 na jingine la Mohammefd Diame la dakika ya 50 yalitosha kuwapa wakati mgumu Sunderland katika janga la kujinasua kushuka daraja kwani imezidi kuwaweka pabaya.
 Bao la kiufutia machozi la wengine lilifungwa dakika ya 65 na Adma Johnson, ambalo hata hivyo halikuweza kuwanasua kutokana nafasi ya pili toka mkiani mwa ligi hiyo inayoelekea ukingoni.

No comments:

Post a Comment