STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 1, 2014

Wema Sepetu, Batuli kupamba tamasha la Kanumba Foundation

Yobnesh Yusuf 'Batuli'
Wema Sepetu 'Madam'
WASANII maarufu wa filamu nchini, Wema Sepetu na Yobnesh Yusuf 'Batuli, ni miongoni mwa wasanii watakaonogesha tamasha la mfuko maalum, utakajulikana kama Kanumba The Great Foundation, litakalofanyika Aprili 7, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Dar Live.
Akizungumza Dar es Salaam jana, mratibu wa tamasha hilo kutoka kampuni ya Vannedrick, George Wakuganda, alisema kuwa
Wema na Batuli wamekubali kushiriki tamasha hilo.
Wakuganda alisema kuwa tamasha hilo litafanyika siku kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Steven Kanumba.
"Wema na Batuli wamekubali kuungana na wasanii wenzao katika tamasha hilo kubwa ambalo litakuwa ni mara ya kwanza kufanyika tangu kifo cha Kanumba," alisema Wakuganda.
Alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri kama yalivyopangwa na kwamba kabla ya siku hiyo kutakuwa na mambo mbalimbali ya kijamii.
Alisema kuwa Jumamosi Aprili 5 wasanii mbalimbali watatembelea hospitali, magereza, vituo vya watoto yatima na kaburi la marehemu Kanumba.
Wakuganda alisema siku ya Jumapili kutakuwa na bonanza maalum ambalo litafanyika kwenye viwanja vya Leaders Club likishirikisha timu 12 za soka.
Alizitaja baadhi ya timu kuwa ni Bandari Veterani, Multi Choice, Boko Veterani, Bongo Movie, Bongo Fleva, NMB, Tanzania Stars, Taswa, Tanzania Stars, CXC Africa na NSSF.
Wakuganda alisema pia kuwa siku ya Aprili 7, kwenye Ukumbi wa Dar Live, patakuwa hapatoshi pale bendi ya muziki wa dansi The African Stars 'wana Twanga Pepeta', pamoja na kundi la muziki wa taarab, Jahazi Morden yatakapotumbuiza.
Alisema kwa upande muziki kipya ni watakaosindikiza watakuwa Snura, TMK Family, Juma Nature, Afande Sele, Babu Ayoub, Tunda Man, Dogo Janja na Linah, huku wasanii wa filamu watakaokuwapo Elizabeth Michael 'Lulu', Patcho Mwamba, Benny Kinyaiya, Aunt Ezekiel, Dude, Wema na Batuli.

No comments:

Post a Comment