STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 1, 2014

Ajali nyingine yachukua uhai wa watu Rufiji


WATU nane wamefariki katika ajali ya majini iliyotokea Mto Rufiji baada ya Mtumbwi kugonga Pantoni na kuzama, ambapo maiti moja kati ya watu hao nane imepatikana.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Rufiji, zinasema kuwa tukio hilo lilitokea Utete majira ya saa 12 jana baada ya nahodha wa mtumbwi huo, Abdallah Yusuf kuzidiwa nguvu na chombo hicho na kulivaa Panton i lililokuwa limeegeshwa kutokana na mto Rufiji kufurika maji.
Taarifa zaidi zinasema watu kadhaa walizama majini na saba kati yao waliokolewa ma wengine nane kutoonekana na kuhisiwa wamekufa majini.
Miongoni mwa waliookolewa ni Ramadhan Mkono, Pili Hungwa, Nasra Magimbi, Shaaban Mbonde, Ramadhani Gido, Karim Salim na Khalid Mbonde. Ikielezwa kuwa watu hao walikuwa wakitoka katika shughuli zao za kila siku.
Wanaodaiwa kufa katika ajali ni ni pamoja na Husna Rwambo, Rubia Rwando, Latifa Mkono, Prisca Kulwa, Diana Kulwa, Uwesu Mbonde, Zaria Mbonde na Mwashamba Chinga.
Ajali hiyo imetokea siku moja baada ya watu 22 kufariki katika ajali ya barabarani wilayani humo iliyohusisha magari matatu, likiwemo basi lililowaparamia waokoaji.

No comments:

Post a Comment