STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

Simanzi tena:Rachel 'Recho' Haule wa Bongo Movie afariki

MUIGIZAJI aliyekuwa anazidi kuja juu katika Bongo Movie, Rachel Haule 'Recho' afariki asubuhi hii Muhimbili Hosp, Dar es Salaam baada ya kujifungua kwa upasuaji, ambapo mtoto alifariki tangu jana.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na muigizaji mwenzake, Zuwena Mohammed 'Shilole', Recho alikumbwa na mauti hayo na kwa sasa wanajipanga kukutana Leaders kwa ajili ya kujua taratibu za mazishi za msanii mwenzao ambaye alikuwa katika hali mbaya tangu alipofanyiwa upasuaji kiasi cha kukimbizwa ICU kabla ya kukumbwa na mauti asubuhi hii.
Kifo cha Recho kimekuja ndani ya wiki moja baada ya kufariki kwa msanii mwingine wa Bongo Movie Adam Kuambiana , huku pia fani ya sanaa ikishuhudiwa ikimpoteza mwanamuziki Amina Ngaluma 'Japanese' aliyefariki nchini Thailand aliyezikwa siku ya Jumamosu.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia ya marehemu Recho na Bongo Movie kwa ujumla kwa kuwataka kuwa na subiora katika kipindi hiki kigumu kwa kutambua kuwa kila Nafsi itaonja Mauti, yeye katangulia sisi tu nyuma yake.

2 comments:

  1. If doable, as you gain expertise, would you mind Spartagen xt updating your webpage with more.formation? It is extremely helpful for me.I think youve produced some actually interesting points. you've got going on in your web site. What is the name of the design by the way? I was thinking of using this style for the blog I am going to make for my school project.Umberto eye reeds Alain soprano rhythm air amnesia.For more ==== >>>>>> http://www.healthcaresups.com/spartagen-xt-exposed/

    ReplyDelete