STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Anti Fifii atengeneza Documentary ya maisha yake, kurusha hewani


NYOTA wa filamu nchini, Tumaini Biligimana maarufu kama Anti Fifii yupo hatua ya mwisho kutengeneza filamu inayohusu maisha yake (documentary) ya kisanii tangu alipoanzia sanaa hiyo mkoani kwa Kigoma hadi alipofikia sasa akiwa ni mtunzi, mwandishi, muongozaji na mtayarishaji.
Akizungumza MICHARAZO, Anti Fifii alisema kuwa kazi hiyo anayoitengeneza kupitia kampuni yake ya See Breeze Art ipo mwishoni kukamilika kabla ya kuanza mchakato wa kusaka mdhamini ili kurushwa hewani katika kituo chochote cha runinga watakachokubaliana nacho.
"Namalizia kutengeneza 'documentary' ya maisha yangu kuanzia nilipotokea kwetu Kigoma hadi kufika nilipo sasa na itarushwa kwenye runinga yoyote baada ya kukamilisha mchakato wa kupata wadhamini," alisema Fifii.
Nyota huyo wa filamu za 'Copy', 'Sound of Death', 'Senior Bachelor', 'I Deserve It', 'Kaburi la Mapenzi', 'Kizungumkuti', 'Fake Smile' na 'Daddy' alisema makala hiyo ya filamu itaenda kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.
Aidha aliongeza kuwa, anafanya mchakato wa kuweka kwenye makala ya filamu, kitabu chake kilichopo mtaani kinachoitwa 'Migogoro ya Ndoa na Suluhisho Lake'.
"Baada ya kukamilisha jambo hili, nitaanza mpango wa kutengenezea makala ya kitabu changu ili irushwe pia kwenye runinga kwa lengo la kuisaidia jamii," alisema.
Anti Fifii alisema anashukuru namna Watanzania walivyokipokea kitabu chake hicho cha kwanza kutunga nje na sanaa yake ya uigizaji aliyoianza miaka 20 Kigoma.

No comments:

Post a Comment