STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Bayern Munich yapumua, Ribery arejea uwanjani

http://multimedia.pol.dk/archive/00430/Germany_Soccer_Bund_430303a.jpg
Franck Ribery
KLABU ya Beyern Munich imepumua baada ya wingawao Franck Ribery kuwa fiti baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu sasa.
Winga huyo anatarajiwa kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wake wa msimu huu wakati timu yake itakapokwaana na VfB Stuttgart kesho Jumamosi.
Ribery amekuwa nje ya uwanja kwa muda kutokana na majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua lakini sasa anaonekana kuwa fiti. 
Mabingwa hao watetezi wameanza kwa kusuasua msimu huu kuliko ilivyokuwa kwa msimu uliopita kufuatia sare ya bao 1-1 dhidi ya Schalke katika mchezo wao wa pili. 
Kwa sasa wasiwasi upo kwa kiungo mpya aliyesajiliwa kiangazi hiki Xabi Alonso ambaye alikosa mazoezi wiki hii kutokana na kuumia mguu na ndio kwanza maenaza kukimbia tena. 
Winga mahiri wa kimataifa wa Uholanzi, Arjen Robben naye pia amefanya mazoezi peke yake kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu wakati beki Rafinha naye akiwa bado nje kutokana na majeruhi ya goti.
Kurejea kwa Ribery ambaye mapema mwezi huu alitangaza kustaafu soka la kimataifa kunakuwa ahueni kubwa kwa Bayern kabla ya mechi yake ya kesho.

No comments:

Post a Comment