STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Simba yalala kwa URA, kesho kuwafuata Ndanda FC

Amri Kiemba akijaribu kuwatoka wachezaji wa URA huku Emmanuel Okwi akiwa tayari kutoa msaada
KLABU ya soka ya Simba imeendeleza uteja wake mbele ya URA ya Uganda baada ya jioni ya leo kunyukwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki la kimataifa lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa.
Simba iliyotoka kuionea Gor Mahia kwa kuilaza mabao 3-0 ilishindwa kupata dawa ya kugeuzwa mteja wa kudumu kwa Watoza Ushuru hao wa Uganda kwa kulazwa bao hilo ikiwa ni mechi ya kwanza kwa Simba kupoteza chini ya kocha Patrick Phiri.
Bao pekee lililoizamisha vijana wa Msimbazi ambayo haijaifunga URA katika mchezo wowote wanaokutana nao iwe kwenye mashindano au mechi za kirafiki liliwekwa kimiani na Frank Kalanda katika dakika ya 42, akimalizia kazi nzuri ya Elkanda Nkungwa.
Kesho asubuhi Simba itapaa angani kuelekea Mtwara tayari kwa pambano lao jingine dhidi ya Ndanda Fc katika kunogesha Siku ya Ndanda (Ndanda Day) linalofanyika kesho kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini humo.

No comments:

Post a Comment