STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Kaole Kwanza waanza mazoezi ya Kipusa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGO1SXfSXqu1qK74H1G9dDqrWDCvkTVNk5T7hq4iyRVPXXngHa5sH7RtZYh62pFiupbwxnCH9w3zgTd5jap6z8OBuU2289az27NUf-V4mONXfcKITG0_B_EBnjRC3Bj3bs6ICLNLtYtYt3/s1600/Kaole1.jpg
Kundi la Kaole Kwanza katika picha ya pamoja siku walipozindua Kipusa chao
KUNDI la Kaole Kwanza ambalo linaoundwa na wasanii waliowahi kutamba na Kaole Sanaa, limeanza tena mazoezi kwa ajili ya kuendelea kurekodi tamthilia yao iitwayo 'Kipusa' ambayo inatarajiwa kuanza kurushwa hewani kupitia runinga.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa viongozi wa Kaole Kwanza, Issa Kipemba alisema baada ya kusitishwa kwa kambi ya mazoezi ili kurekebisha mchakato wa kusaka kituo cha kurushia mchezo wao, hatimaye mazoezi hayo yameanza tena.
Kipemba alisema wanafanya mazoezi hayo kabla ya kuendelea kurekodi kazi hiyo tayari kwa kuanza kurushwa na moja ya vituo vya televisheni nchini ambacho hata hivyo hakupenda kukitaja jina kwa sasa kwa madai ni mapema mno.
"Muda ukifika wa kuanika jina la kituo hicho tutaweka bayana, ila tumeshaanza mazoezi ili kuendelea na kurekodi tamthilia yetu ya 'Kipusa' tuliyoizindua kwa mashabiki mapema mwaka huu," alisema Kipemba.
Kundi hilo linaloongozwa na Ndimbagwe Misayo Thea, linaundwa na wakali kama Muhogo Mchungu, Bi Hindu, Swebe Santana, Bi Staa, Bi Terry, Kingwendu, Davina na wengine.

No comments:

Post a Comment