STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Pele asema Messi ananafasi ya kutwaa Kombe la Dunia

http://i.lidovky.cz/10/042/lnc460/ANT326be7_pele_messi.jpg
GWIJI wa soka wa Brazil, Pele amesema kwamba Lionel Messi bado anayo nafasi ya kutwaa Kombe la Dunia na kuongeza kwamba nyota huyo wa Barcelona tayari ni mmoja wa magwiji wa soka hata kama atashindwa kuiongoza Argentina kutwaa taji hilo.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alikaribia kubeba Kombe la Dunia wakati alipoiongoza Argentina kufika fainali nchini Brazili, lakini likatua kwa Ujerumani walioshinda katika muda za ziada.
Licha ya hivyo, Pele ameweka wazi kwamba Messi bado anayo nafasi na anaamini kwamba atapata fursa nyingine ya kutwaa tajihilo 2018.
"Hakika, Messi bado anaweza kutwaa Kombe la Dunia," Pele aliiambia DPA.
"Messi ni mchezaji aliyekamilika na yuko katika hali nzuri sana kimwili. Sina shaka kwamba bado atatamba kwenye Kombe la Dunia.
"Kufungwa katika fainali Brazil hakumuondolei ukweli kwamba Messi ni mchezaji mkubwa sana. Atapata fursa nyingine ya kutamba nchini Russia.
"Hakuna shaka kwamba Messi ni bonge la mchezaji. Hatuwezi kuhoji uwezo wake kwa sababu tu hajatwaa Kombe la Dunia bado."
Messi amecheza mechi 93 za timu yake ya taifa na ameifungia magoli 42.

No comments:

Post a Comment