STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 12, 2014

Yazidu, Mualgeria kuzipiga leo Kilimanjaro

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjV3aoPNkQStbdya_xo9DDga_uJKAZONafyPywYx0IFQ9HWB7SawEnKhtxexF4oelIE9Lh6oDZ0boQqW0eMbWmi2A0pKrzwcbdX-ENAE9gZbMY8G-JDW69mvsv_K78nfdqdKonJ8QNLH2t9/s1600/IMG_1831.JPG
Said Yazidu (kushoto) ma Dahou wakiinuliwa mikono jana walipomaliza kupima uzito
BONDIA mkongwe nchini Said Yazidu wa Tanzania na Djamel Dahou kutoka Algeria wanatarajia kuonyeshana kazi leo kwenye pambano la kuwania Ubingwa wa Dunia wa UBO katika pigano litakalofanyika mjini Moshi, Kilimanjaro.
Tayari Dahou ameshatua nchini tangu juzi tayari kwa pambano hilo la raundi 12 ambalo litafanyikia kwenye ukumbi wa YMCA, mjini Moshi na kusindikizwa na michezo mingine kadhaa ya utangulizi likiwemo la kuwania ubingwa wa UBO Afrika.
Mabondia wote wanaopanda ulingoni leo wamepimwa afya na uzito jana na wameonekana fiti tayari kurushiana makonde.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Anthony Rutta, pambano hilo la ubingwa wa Afrika litahusisha mabondia  Mtanzania Ali Ramadhan 'Alibaba' dhidi ya Mmalawi, Alick  Mwenda.
Ruta alisema mapambano yote hayo yameandaliwa na kampuni ya Green Hill Promotion na ni fursa nzuri ya kufufua ngumi za kulipwa katika mkoa wa Kiliamanjaro.
"Mpinzani wa Said Yazidu, Djamel Dahou ameshatua na anaelekea Kilimanjaro kwa ajili ya pambano lao la Septemba 12 kwenye ukumbi wa YMCA," alisema.
Rutta alisema pambano hilo litatanguliwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiwamo la UBO Afrika la raundi 10 kati ya Alibaba na Mwenda wa Malawi.
Mengine ni kati ya Fatuma Yazidu dhidi ya Joyce Adam, Emmanuel Alex dhidi ya Ali Bugingo huku Pascal Bruno atazipiga na Cosmas Kibuga, George Allen atazipiga na Ssebo Husseni na Raymond Bwango dhidi ya Fadhil Mkinda.

No comments:

Post a Comment