STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 13, 2014

Diego Costa, kocha wa Swansea City funika bovu England

Diego Costa akiwa na tuzo yake
Kocha wa Swansea, Garry Monk akiwa na tuzo yake ya Mwezi Agosti
STRIKA mpya wa Chelsea, Diego Costa ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Agosti wa Ligi Kuu ya England, huku kocha wa Swansea Garry Monk akiinyakua tuzo kama hiyo kwa upande wa makocha.
Mpachika mabao huyo aliyetokea Atletico Madrid aliyefunga mabao manne katika mechi tatu walizocheza Chelsea ameianza ligi hiyo kwa mguu wa bahati.
Wakati Costa akiing'ara hivyo, kwa upande wa  Garry Monk, Kocha wa Swansea aliwafunika makocha wenzake kadhaa baada ya kushinda tuzo ya mwezi Agosti.
Kocha huyo ameshinda tuzo ya kocha bora wa mwezi huo baada ya kuiwezesha timu yake kushinda mechi zake zote tatu, ikiwemo dhidi ya Manchester United Uwanja wa Old Trafford. 

No comments:

Post a Comment