STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 14, 2014

Real Madrid yafa nyumbani, Neymar aibeba Barcelona La Liga


Atletico Madrid's Arda Turan scores
Kitu hicho! Atletico Madrid wakiwaadhibu wenyeji wao
Cristiano Ronaldo
Hawaamini kama ni kweli wamepigwa
Cristiano Ronaldo scored a penalty in Real Madrid's 2-1 defeat against Atletico Madrid on Saturday
Ronaldo akifunga mkwaju wake wa penalti
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Hispania, Atletico  Madrid wameendeleza ubabe wake kwa Real Madrid baada ya kuinyuka  mabao 2-1 Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, katika mchezo wa ligi hiyo.
Atletico waliwashtukiza wenyeji wao kwa kuandika bao la kuongoza dakika ya 10 tu ya mchezo huo kupitia kwa Tiago.
Wenyeji walicharuka na kusawazisha dakika sita baadaye kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa penalti na kufanya hadi mapumziko mambo yawe 1-1.
Atletico walirejea tena nyavuni mwa wenyeji wao kwa kuandika bao la pili na la ushindi katika dakika ya 76 kupitia kwa Arda Turan aliyemaliza kazi nzuri ya Raul Garcia. 

Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Barcelona walipta ushindi nyumbani dhidi ya Athletico Bilbao kwa kuwalaza mabao 2-0.
Mabao yote ya wenyeji wakiwekwa kimiani katika kipindi cha pili na nyota wa Kibrazil, Neymar.
Ijumaa timu za Almeria na Cordoba zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, wakati katika mechi nyingin e za jana,Malaga na Levante zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu huku Celta Vigo na Real Sociedad zikitoka 2-2.

No comments:

Post a Comment