STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 14, 2014

Simba yabanwa na Ndanda Fc Mtwara

Simba SC
Ndanda Fc
SIMBA imeendelea kwenda mwendo wa kusuasua katika mechi zake za kujiandaa kwa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya jana kulazimishwa kutoka suluhu na Ndanda FC.
Katika mechi hiyo ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, vijana wa Ndanda waliwabana vyema wapinzani wao katika vipindi vyote viwili.
Sare hiyo imekuja siku chache baada ya Simba kuchapwa bao 1-0 na URA ya Uganda katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kama ilivyokuwa katika mechi dhidi ya URA, mshambuliaji Emmanuel Okwi alishindwa kuonyesha makeke yake kutokana na kubanwa vyema na mabeki wa Ndanda. Okwi aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Abdalla Seseme.

No comments:

Post a Comment