STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 5, 2014

Liverpool yazinduka England, Sunderland yaua

Jordan Henderson (kulia) akishangilia bao lake la pili baada ya kufanya 2-1 dhidi ya West Brom AlbionTIMU ya Liverpool imezinduka kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 nyumbani dhidi ya West Bromwich Albion.
Mabao ya washindi yalifungwa na Adam Lallana na Jordan Henderson, wakati lile la wageni lilifungwa kwa mkwaju wa penati na  Saido
Berahino. 
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Hull City ikiwa nyumbani iliitambia Crystal Palace kwa mabao 2-0, huku Leicester City ikibanwa kwao kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Burnley.
Nayo Sunderland ikiwa nyumbani iliiua Stoke City kwa kuizamishwa kwa mabao 2-1 na Swansea City kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Newcastle United.

No comments:

Post a Comment