![]() |
Falcao akishangilia bao lake lililokuwa la pili kwa Mashetani Wekundu mapema leo |
![]() |
Di Maria akishangilia bao la kwanza la Man Utd ambalo ni la tatu kwake tangu ajiunge na timu hiyo |
![]() |
Erikson akiifungia Spurs bao dhidi ya Southampton |
![]() |
Radamel Falcao akishangilia bao lake la kwanza tangu ajiunge Old Trafford |

Angel
Di Maria akishangilia baada ya kufunga goli la uongozi la Manchester
United dhidi ya Everton kunako dakika ya 27 hili likiwa ni goli lake la
tatu tangu kujiunga United

Wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford, Mashetani Wekundu walionyesha dhamira ya ushindi kwa kuandika bao la kwanza lililofungwa na Di Maria dakika ya 27 akimalizia pasi ya Juan Mata.
Bao hilo lililodumu hadi mapumziko kabla ya wageni kuchomoa kupitia kwa Naismith katika dakika ya 55 kama ya nyota wa zamani wa Atletico Madrid na Monaco Falcao kufunga bao la ushindi dakika ya 62 kwa kazi nzuri iliyofanywa na di Maria na kuwapa ushindi muhimu vijana wa Luis Van Gaal.
Katika pambano jingine la ligi hiyo Tottenham Hotspur ikiwa uwanja wa nyumbani wa White Hartlane walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Southampton.
Bao pekee la pambano hilo lilifungwa na Christian Eriksen dakika ya 40 na kuwafanya Spurs kupata ushindi muhimu na pointi tatu zilizowafanya kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya sita.
No comments:
Post a Comment