STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 5, 2014

Manchester Utd, Spurs zaua England, Di Maria achaa bwana!

Radamel Falcao
Falcao akishangilia bao lake lililokuwa la pili kwa Mashetani Wekundu mapema leo
Angel di Maria celebrates
Di Maria akishangilia bao la kwanza la Man Utd ambalo ni la tatu kwake tangu ajiunge na timu hiyo
Tottenham playmaker Christian Eriksen (left) rifles in a shot to put his side in front against Southampton
Erikson akiifungia Spurs bao dhidi ya Southampton

Radamel Falcao akishangilia bao lake la kwanza tangu ajiunge Old Trafford
Angel Di Maria celebrates scoring Manchester United's first goal against Everton on 27 minutes - it was his third goal in a United shirt
Angel Di Maria akishangilia baada ya kufunga goli la uongozi la Manchester United dhidi ya Everton kunako dakika ya 27 hili likiwa ni goli lake la tatu tangu kujiunga United
Di Maria celebrated by replicating the heart-shaped celebration of his former Real Madrid colleague Gareth Bale
MABAO mawili kutoka kwa wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni, Angel di Maria na Radamel Falcao yameisaidia Manchester United kuchupa hadi nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu England baada ya kuilaza timu ya Everton kwa mabao 2-1.
Wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford, Mashetani Wekundu walionyesha dhamira ya ushindi kwa kuandika bao la kwanza lililofungwa na Di Maria dakika ya 27 akimalizia pasi ya Juan Mata.
Bao hilo lililodumu hadi mapumziko kabla ya wageni kuchomoa kupitia kwa Naismith katika dakika ya 55 kama ya nyota wa zamani wa Atletico Madrid na Monaco Falcao kufunga bao la ushindi dakika ya 62 kwa kazi nzuri iliyofanywa na di Maria na kuwapa ushindi muhimu vijana wa Luis Van Gaal.
Katika pambano jingine la ligi hiyo Tottenham Hotspur ikiwa uwanja wa nyumbani wa White Hartlane walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Southampton.
Bao pekee la pambano hilo lilifungwa na Christian Eriksen dakika ya 40 na kuwafanya Spurs kupata ushindi muhimu na pointi tatu zilizowafanya kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya sita.

No comments:

Post a Comment