STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 26, 2014

Mtibwa Sugar, Mbeya City mechi ya kisasi uwanja wa Sokoine

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjlJf64SG64DfJN7BM-53k1KlucFsKrbFxFr_y5V-f-hzeuQHd37uiyn1X55N4JDkul86QALQo4LvdhfS4A9-2LdeKlRwNXFFZlpBVrKjaLiYBNJ_ccp2G3hMRm-61qTTcPZD0bsP8LaUnA/s1600/IMG-20140920-WA0053.jpg
Mbeya City
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYmJd6ab_qzfQWniaUmNB3Pd4CdjKmz11F2TFKEd9xYoQI9SkaMJQhqFApjnnTw0KNhZXUSZJXq4gneRPGFKhIhuwMQSNvfMzwe4Ci_DzU_U6Psbf27VJgMpXXMt-Ocpqru7qeI9FKPvxr/s1600/MTIBWA+SUGAR+2014.JPG
Mtibwa Sugar
BAADA ya kutolewa nishai kwenye uwanja wa nyumbani na mabingwa watetezi, Azam kwa kulazwa bao 1-0, Mbeya City leo itakuwa na kibarua kingine kigumu wakati watakapowakabili Mtibwa Sugar kwenye uwanja huo wa Sokoine, Mbeya.
Timu hiyo itawakaribisha Mtibwa inayoonekana kuwa fiti zaidi msimu huu katika pambano la kuhitimisha raundi ya tano wikiendi hii.
Mbeya City iliyoweka rekodi ya aina yake msimu uliopita kwa kupanda daraja na kumaliza msimu wakiwa nafasi ya tatu ilikuwa haijafungwa bao lolote wala kupoteza mchezo kabla ya mechi iliyopita dhidi ya Azam na kumfanya kocha Juma Mwambusi kukuna kichwa kuweza kurejesha makali ya kikosi chake kilichojijengea jina kubwa katika soka nchini.
Tofauti na msimu uliopita ambao walichuana na Azam kuwa miongoni mwa timu ambazo zilikuwa hazijapoteza mchezo mpaka Yanga walipowatibulia, Mbeya City inalazimika leo kupata ushindi ili kujiweka pazuri katika mbio za kuwania ubingwa, ingawa Mtibwa Sugar ya msimu huu haitabiriki kwa kuwa na makali kama miaka iliyonyakua ubingwa mara mbili.
Mtibwa ambayo jana ilirejea kileleni mwa msimamo baada ya Azam kufungwa bao 1-0 na JKT Ruvu imetamba kuwa imeenda Mbeya kwa lengo moja tu la kushinda ili kuzidi kujiongezea pointi za kutwaa ubingwa msimu huu sambamba na kulipa kisai cha mabao 2-1 ilichopewa kwenye uwanja huo msimu uliopita.

Kocha wa Mtibwa, Mecky Mexime ametamba wameenda Mbeya kukusanya pointi kabla ya kuwasubiri Simba wiki ijayo watakaoumana nao uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Mexime nahodha wa zamani wa Mtibwa na Taifa Stars, alisema suluhu waliyopata kwa Polisi hawakuifurahia, hivyo wanajipanga kuhakikisha wanapotezi tena pointi kizembe ili kutimiza lengo la kutwaa ubingwa msimu huu.
Kikosi hicho cha wakata miwa walianza msimu huu kwa kishindo kwa kuilaza Yanga mabao 2-0 kabla ya kuja kuifumua 'wageni' wa ligi hiyo Ndanda Fc kwa mabao 3-1 na kisha kuizima Mgambo JKT kwa bao 1-0 na kukusanya pointi 10 baada ya mechi nne, wakati wapinzani wao wana pointi tano kutokana na mechi nne walizocheza.
Mbeya City walianza kwa kutoka suluhu na JKT Ruvu kabla ya kuilaza Coastal Union bao 1-0 na kutoka tena suluhu ya Ruvu Shooting kabla ya kulala kwa Azam.
Katika mechi baina yao kwa msimu uliopita, Mtibwa na Mbeya Cirty zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyocjhezwa uwanja wa Manungu, Morogoro kabla ya Mbeya City kushinda mabao 2-1 uwanja wa Sokoine katika marudiano.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P    W    D   L    F    A   GD  Pts
01. Mtibwa Sugar    04  03  01  00  06  01  05  10
02. Azam                05  03  01  01  06  02  04  10
03. Yanga               05  03  01  01  07  04  03  10
04. Coastal Union   05  02  02   01  07  05  02  08
05. JKT Ruvu          05  02  01  02   04  05  -1  07
06. Ruvu Shooting  05  02  01   02  04  05  -1  07
07. Kagera Sugar    05  01  03   01  04  03  01 06
08.  Mgambo JKT    05  02  00  03   02  04  -2  06
09. Prisons              05 01  02   02  05  05  00  05
10. Simba               05  00  05   00  05  05  00 05
11. Mbeya City        04  01  02  01   01  01  00  05
12. Stand Utd          05 01  02   02  03   08  -5  05
13. Ndanda Fc         05  01  00  04   07  10  -3  03
14. Polisi Moro         05  00  03  02   03  06  -3  03

No comments:

Post a Comment