STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Maokola, MP Minoma kumaliza ubishi Desemba 19

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2DnzKJGvRGtEhB1V2Y09n6CRWs1Qt2k8RO129VGkP8domwzd7Qm7S2j22fN_8byoAanbCE1dOXeQuGqyfZL8iyAHSvvq8FQcnkAuxOo_2eVfUR0EAtGwI2zAtLZxL8f51cHY02Lq5eXTB/s1600/IMG_0408.JPG
Maokola na Mkalakala watakaorudiana tena kuwania ubingwa wa TPBC
BINGWA wa ngumi za kulipwa wa uzito wa Light Middle anayetambuliwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Ibrahim Maokola anatarajiwa kupanda ulingoni Desemba 19, mwaka huu kwa ajili ya kutetea ubingwa wake huo dhidi ya Seleman Mkalakala 'MP Minoma'.
Rais wa TPBC, Chaurembo Palasa aliliambia MICHARAZO kuwa pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 na litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi, litachezwa kwenye Ukumbi wa Vigae Pub, Mbagala Dar es Salaam.
Palasa alisema sababu ya kupeleka pambano hilo Mbagala ni kutaka kuhamasisha mchezo huo wa ngumi katika maeneo mengine badala ya kuendelea kuchezwa katika kumbi zile zile zilizozoeleka.
"Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), tumeidhinisha pambano la ngumi kati ya Ibrahim Maokola atakayekuwa akitetea taji lake dhidi ya Seleman Mkalakala, mchezo huo utasindikizwa na michezo mingine kadhaa ya utangulizi," alisema Palasa.
Palasa alitaja baadhi ya michezo ya utangulizi kuwa ni lile la wapinzani wa jadi, Abdallah Mohammed 'Prince Nassem' dhidi ya Salehe Mkalekwa.
"TPBC inataka kuleta mvuto kwa mchezo huo kwa kupelekwa katika maeneo mengine nje ya kumbi zilizozoeleka, ili kuwavutia wadhamini sambamba na kuhakikisha vipaji vipya vinaibuka ndani na nje ya jijini la Dar es Salaam ili kuendeleza ngumi," alisema Palasa.
Aidha, Palasa alitoa tahadhari kwa mabondia, waratibu na mapromota ambao watakiuka sheria na kanuni za mchezo kuwa watachukuliwa hatua kali za kinidhamu ili kuhakikisha ustaarabu unaendelea kuwepo katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment