STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Chelsea kumpa kibarua cha kudumu Drogba

Mourinho akiwa na Drogba
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema mshambuliaji wake Didier Drogba bado atakuwa na kazi Stamford Bridge wakati akiamua kustaafu rasmi kucheza soka. 
Drogba mwenye umri wa miaka 36 kwasasa anaichezea kwa mara ya pili klabu hiyo huku akifunga bao katika mchezo wa jana ambao Chelsea waliibugiza Tottenham Hotspurs kwa mabao 3-0. 
Akihojiwa Mourinho amesema jambo ni kwamba nyota huyo atamalizia soka lake akiwa na Chelsea na inavyoonekana anaweza kubakia akifanya mambo mengine pindi atakapostaafu. 
Drogba amefanikiwa kushinda mataji 10 akiwa na Chelsea mara ya kwanza kati ya mwaka 2004 mpaka 2012 huku akifunga mabao 157 katika mechi 341 alizocheza. 
Nyota huyo alijiunga tena na Chelsea katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka huu baada ya kuondoka klabu ya Galatasaray ya Uturuki.

No comments:

Post a Comment