STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Zahoro Pazi kumbadili Mrwanda Polisi Moro

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgeIFO6Ts0oOYH-zSbZQpHtdE3LBHVEuBeH3qRPbnGO4jkbsbTrXqiLajnsS3YTyKidqQxsd0gZR9d434iV_lBuB4lrqz1F_FDTjFIQMRqaHqCmd338YusINEHVosFi2MAeESOCzguCrgXd/s1600/pazi.JPG
Zahoro Pazi alipokuwa Simba
TIMU ya Polisi ya Morogoro inayoshiriki Ligi Kuu imemsajili mshambuliaji wa Simba, Zahor Pazi, mtoto wa kipa wa zamani wa wekundu hao, Idd Pazi 'Father' katika kipindi hiki cha dirisha dogo linalotarajiwa kufugwa Desemba 15, mwaka huu.
Zahor ambaye anacheza nafasi ya ushambuliaji, amesaini mkataba wa kuichezea timu ya Polisi ya Morogoro kwa kipindi cha mwaka mmoja katika ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa, ambaye pia ni mlezi wa timu hiyo.
Hatua ya Polisi kumsajili mchezaji huyo ni kujibu mapigo baada ya timu ya Simba kuwa mbioni kumsajili mshambualiaji wao tegemeo, Danny Mrwanda.
Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa timu hiyo ya Polisi, Issa Bushir alisema kuwa wameamua kumchukua mshambuliaji huyo kutokana na uwezo alionao na kwamba wanaamini kuwa ataisaidia timu hiyo katika ligi inayotarajiwa kuendelea wiki mbili zijazo.
Naye mlezi wa timu hiyo ya Polisi, ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonald Paul, alisema wanaamini mshambuliaji huyo ataweza kuziba pengo la Mrwanda anayehamia timu ya Simba.
Kwa upande wake Zahor alihaidi wanachama na wapenzi wa timu ya Polisi Morogoro kuwa atajituma kwa kushirikiana na wachezaji wenzake ili kuiletea ushindi timu hiyo ya 'maafande'.

No comments:

Post a Comment