STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Simba, Yanga kula shushu Mtani Jembe, viingilio vyatajwa

Vikosi vya Simba na Yanga
KLABU za Simba na Yanga watapata nafasi ya kubadili hadi wachezaji watano katika mechi ya kirafiki ya Bonanza, maarufu kama Mtani Jembe, ambayo viingilio vya mechi hiyo vimkitangazwa hadharani.

Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura amesema wamefikia uamuzi huo kuwa wachezaji wanaoruhusiwa kuingia katika dakika 90 ni hadi watano kwa kila timu.
“Sub imeongezwa siku hiyo, badala ya wachezaji watatu, itakuwa hadi wachezaji watano.
“Kama mechi itaisha ndani ya dakika tisini bila ya kupata mshindi, basi zitapigwa penalti tano tano kwanza.
“Kikubwa katika mechi hiyo ni lazima siku hiyo mshindi apatikane,” alisema Wambura.
Wambura alisema pambano hilo litachezwa kwa dakika 90 tu na kama muda huo hatapatikana mshindi, mikwaju ya penalti itatumika na kwamba mshindi na marefa watakaolisimamia wanatarajiwa kutajwa leo na Kamati ya Waamuzi ya shirikisho.
Pia aliweka bayana viingilio vya mechi hiyo ya Jumamosi ijayo kuwa kiingilio cha chini kitakuwa Sh 7000 na cha juu Sh 30,000.

"Viingilio vya mechi hiyo ni Sh. 30,000 kwa VIP B, Sh. 20,000 kwa VIP C, 15,000/- kwa viti vya rangi ya chungwa na Sh. 7,000 kwa viti vya bluu na kijani. Tiketi zitakazotumika ni za kawaida na zitauzwa kwenye vituo ambavyo vitatangazwa baadaye," alisema Wambura.Mechi hiyo ya Bonanza inasubiriwa kwa hamu kubwa.

No comments:

Post a Comment