STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Tom Oloba apewa jukumu ya kunasa msaidizi wa Mombeki

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYcQ4GKfL84y4L09fZetG_9-iVLkU_gy6fWn9b2LjkoG-I89l_VehzDBlZEEPOxfcGAfGdq90_0rMu0KqwI3yOU4rTJc6B2UkJ6pWcErF0K-kEibqKmTapUgHCgW67ki5XFunEQjgRTfQ/s1600/IMG_6927.JPG
Mombeki alipokuwa Simba
UONGOZI wa klabu ya Ruvu Shooting, umesema hatma ya mshambuliaji mpya wa pili anayehitajiwa na kikosi chao ipo mikononi mwa kocha wao Tom Olaba, kwani tayari wachezaji zaidi ya watatu wanaendelea kufanyiwa majaribio kwenye mazoezi ya timu hiyo.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire alisema baada ya kumsainisha mkataba wa mwaka mmoja mshambuliaji wa zamani wa Simba, Betram Mombeki kwa sasa wanasaka mchezaji wa mwisho na tayari chipukizi kadhaa wanafanyiwa majaribio kabla ya kocha Oloba kuamua.
Bwire alisema, Mkenya Olaba ndiye mwenye jukumu la kuamua nani anayemfaa katika kikosi chake kama alivyoamua kwa Mombeki ambaye alisainishwa mkataba wake mapema wiki hii.
"Tumefanikiwa kumnasa Mombeki na sasa kocha anaendelea kuwapima wachezaji waliojitokeza kwenye mazoezi, atakayemfaa ndiye atakayetueleza tumsainishe kwa ajili ya kukipa katika timu yetu, ila tunaamini tutafunika ligi ikiendelea kwa namna kikosi chetu kinavyoendelea kujifua," alisema.
Bwire alisema timu yao ipo kambi ya mazoezi tangu Novemba 24 na walianza mapema kwa ajili ya kutoa nafasi kwa kocha wao kurekebisha mapungufu yaliyoiangusha timu kwenye mechi za raundi saba zilizopita ambapo timu hiyo ilijikuta ikienda mapumziko wakiwa kwenye nafasi ya 11 kati ya timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo kwa kukusanya pointi saba tu.
Ruvu inatarajiwa kuendelea na ligi Desemba 28 kwa kuvaana na ndugu zao wa JKT Ruvu wanaonolewa na kocha Fred Felix Minziro wanaokamata nafasi ya sita wakiwa na pointi 10.

No comments:

Post a Comment