STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Robbie Keane ang'ara Marekani

http://www.trbimg.com/img-547ffbde/turbine/la-sp-keane-mls-mvp-20141204-001/500/500x281MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Los Angeles Galaxy Robbie Keane ametajwa kuwa mchezaji mwenye thamani zaidi maarufu kama MVP katika Ligi Kuu ya Soka nchini Marekani-MLS kwa mwaka huu. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Ireland amefunga mabao 19 katika mechi 29 hivyo kuwapita washambuliaji wengine akiwemo Lee Nguyen wa New England Revolution na Obafemi Martins wa Seattle Sounders. Akihojiwa Keane amesema hakwenda nchini Marekani kwa ajili ya likizo bali kufanya kazi hivyo anafurahi kunyakuwa tuzo hiyo. 
Keane mwenye umri wa miaka 34 ambaye ndiye mfungaji mwenye mabao mengi katika timu yake ya taifa aliendelea kudai kuwa bado anapenda kuendelea kucheza kwa kiwango cha juu.

No comments:

Post a Comment