STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Simba kuivaa Express bila Mkude, Sserunkuma ndani

Dan Sserunkuma anayeterajiwa kuonekana na uzi mwekundu leo
Kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani leo dhidi ya Express
MSHAMBULIAJI wa Simba Jonas Mkude anatarajia kuikosa mechi ya leo ya majaribio dhidi ya timu ya The Express  kutoka nchini Uganda kutokana na kuwa majeruhi, huku pia Dan Sserunkuma akitarajiwa kuonekana uwanjani na timu hiyo kwa mara ya kwanza.
Akizungumza jana Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri alisema, Mkude, Ivo Mapunda na Hussein Shariff 'Casilas' wote wataikosa mechi hiyo ambayo ni muhimu kwa timu kujipima uwezo kabla ya mchezo wa 'Nani Mtani Jembe 2' dhidi ya Yanga Desemba 13, mwaka huu.
"Mechi ya leo ni muhimu kwetu, kwa sababu itatuonesha kipimo cha wachezaji kabla ya mchezo wetu wa Nani Mtani Jembe dhidi ya watani wetu Yanga,"alisema Phiri.
Alisema lengo la mchezo huo ni pamoja na kujiweka sawa kabla ya mchezo huo na Yanga na ule wa mzunguko wa nane wa Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 26, mwaka huu katika viwanja tofauti hapa nchini.
Alisema mchezo huo pia utatumika kumpima mchezaji kutoka Gambia Omary Mboob ambaye anafanya majaribio kwa ajili ya kusajiliwa katika dirisha dogo la usajili linalofikia ukingoni Desemba 15, mwaka huu.
Akizungumzia mazoezi kwa ujumla alisema yanaendelea vizuri ambapo alisema wachezaji wameonyesha moyo wa kujituma pale wanapokuwa uwanjani kuendelea na mazoezi.

No comments:

Post a Comment