STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 5, 2014

Pellegrini amvulia kofia kun Aguero

KOCHA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amemmwagia sifa lukuki mshambuliaji wake Sergio kun Aguero akisema ni mmoja kati ya wachezaji watano bora duniani.
Meneja huyo aliyasema hayo baada ya mshambuliaji huyo wa Argentina, kuisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Sunderland juzi. 
Katika mchezo huo City walitoka nyuma na kufanikiwa kushinda mchezo huo muhimu kwa kufunga mabao mawili na kumfanya Aguero kufikisha jumla ya mabao 14 msimu huu. 
Pellegrini amesema anadhani Aguero yuko katika orodha ya wachezaji watano bora duniani na kwa umri wa miaka 26 alionao bado ana nafasi ya kuimarika zaidi. 
Mbali na Aguero, kocha huyo pia aliwapongeza viungo wake Yaya Toure na Samir Nasri kwa juhudi zao kubwa kuhakikisha wanajiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment