STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 28, 2015

Baby Madaha atambia Saint and Ghost

MUIGIZAJI nyota wa filamu na muimbaji wa muziki wa Bongofleva, Baby Madaha, ametamba kuwa filamu yake mpya anayoianda kwa sasa iitwayo 'Saint and Ghost' ni kati ya kazi zitakazoleta mapinduzi makubwa nchini katika ulimwengu wa filamu.
Madaha, alisema filamu hiyo ambayo inawashirikisha nyota mbalimbali nchini akiwamo yeye mwenyewe (Madaha) ni kati ya filamu za kusisimua ambazo hazijawahi kutengenezwa nchini kutokana na msuko wa simulizi lake.
"Hata aina ya wasanii walioshiriki ni vichwa kwelikweli kitu kinachoifanya filamu hiyo kuwa ya kipekee, alisema Madaha.
Madaha aliwataja wasanii walioshiriki kazi hiyo iliyozalishwa chini ya kampuni yake ya DarkAngel Film Production & Entertainment ni pamoja na Kulwa Kikumba 'Dude', Hidaya Njaidi,  Grace Mapunda 'Mama Kawele', Ramadhani Ally 'Tafu', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo' na wengine.
Kabla ya filamu hiyo Madaha, alicheza filamu kama 'Nani', 'Misukosuko3', 'Mpishi', House Na.44' na 'Ray of Hope' iliyompa tuzo kadhaa ikiwamo ya ZIFF na African Movie.

No comments:

Post a Comment