STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 28, 2015

C.P.U kutinga Uganda kufuatilia mkasa wa mtoto aliyeteswa

WARATIBU wa Filamu ya kutetea watoto ya  C.P.U iliyoshirikisha nyota mbalimbali nchini na ambayo itakuwa ikitolewa kwa mtindo wa matoleo (episode) wanatarajiwa kutinga nchini Uganda kwa ajili ya kufuatilia mkasa wa 'hausi gel' aliyefungwa nchini humo kwa sababu ya kumfanyia kitendo cha ukatili mtoto wa bozi wake.
Filamu hiyo iliyotungwa na Stanford Kihore na kuandikwa na Novatus Mgulusi 'ras' imetengenezwa  kwa ushirikiano wa kampuni mbili za kitanzania za Haak Neel Productions na Wegos Works Ltd ilizinduliwa mwaka juzi na kuanza kuonyeshwa kwenye majumba ya sinema kabla ya sasa kuandaliwa katika mtindo wa DVD ili kuonwa na watu mbalimbali ndani na nje ya nchi,.
Wakizungumza na MICHARAZO waratibu wa filamu hiyo walisema kuwa kwa sasa filamu hiyo ina kuendelezo wa sehemu ya kwanza na itakuwa na matoleo 16 yanayohusu namna ya kukabiliana na unyanyasaji na ukatili kwa watoto.
Waratibu hao walisema kuwa, mwandishi wa C.P.U, Ras Mgulusi anatarajiwa kwenda nchini Uganda kuongea na familia ya mtoto aliyefanyiwa tukio baya na msichana wa kazi kupigwa na kutupwa chini kisha kupigwa mateke sambamba na kufanya mahojiano msichana huyo ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka minne kwa kosa hilo ili kutambua kilichomfanya afanye unyama ule.
"Lengo kubwa ni katika kuboresha na kuliweka tukio hilo ndani ya filamu hiyo ya CPU, ambayo ni kitendo maalum cha kutetea watoto ikiwa imeshirikisha nyota mbalimbali nchini," taarifa ya waratibu wa filamu hiyo inasomeka.
“Nilikuwa nafuatilia ripoti ya Unisef kuhusu taarifa za unyanyasaji wa Watoto kitu kilichonigusa na kuamua kuandika filamu ambayo inaweza kuwa ni dira na mwongozo wa jamii kukwepa au kuwasaidia watoto wanaonyanyaswa katika familia zao,”alisema Ras Mgulusi.
Filamu hiyo imeshirikisha zaidi ya wasanii 100 baadhi yao ni; Kulwa Kikumba ‘Dude’ Illuminata Posh 'Dotnata', Richard Mshanga ‘Mzee Masinde’, Hashim Kambi ‘Ramsey’, Sauda Simba, Subira Wahure, Steve Sandhu 'Pride', Nkwabi Juma, Mohamed Fungafunga ‘Mzee Jengua’ Mobby Mpambala ambao ndiyo vinara wake.
Kwa mujibu wa warartibu hao filamu hiyo inatarajiwa kuwa sokoni kuanzia mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment