STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 28, 2015

Hammer Q mkewe wajipanga kutoa mpya

MKALI wa miondoko ya mduara, Hussein Mohammed 'Hammer Q' pamoja na mkewe Salha Abdallah 'Salha wa Hammer' wanatarajia kuachia wimbo wao mpya wa 'Safiri Salama' ikiwa ni muendelezo wa maandalizi ya kutoa albamu yao kamili.
Akizungumza na MICHARAZO, Hammer Q alisema kazi hiyo mpya ambayo imesharekodiwa kitambo itaachiwa mara baada ya kumalizika kwa maonyesho ya sherehe za miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Nyumba ya Vipaji Tanzania (THT).
Hammer Q, alisema mpaka sasa wamefanikiwa kutoa wimbo mmoja wa 'Wapendanao' ambao umekuwa ukifanya vema kwenye vituo vya redio na kwamba utakaofuata ni 'Safiri Salama' kabla ya kumalizia kurekodi nyimbo nyingine za albamu hiyo inayaokuwa na nyimbo tano.
"Kwa sasa tupo bize na sherehe za miaka 10 ya THT, baada ya hapo tutaachia wimbo wetu wa pili kabla ya kumalizia albamu ambayo tumepanga kuitoa kabla ya Juni mwaka huu," alisema Hammer Q.
Msanii huyo aliwahi kutamba kwenye Bongofleva kupitia wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye miondoko ya taarab akipitia makundi kadhaa likiwamo la Dar Modern, Five Star, na TOT taarab.

No comments:

Post a Comment