STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 28, 2015

Mbeya City 'yaua' Mnyama Taifa, Chollo akosa penati

mbeyacityfc 1-4 vipers fc_2014_1
Mbeya City
IMG_6078 (2)
Simba
KLABU ya Simba jioni ya leo imewanyima raha mashabiki wake baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mbeya City, huku ikishuhudiwa timu hiyo ikipoteza nafasi ya kuasawazisha bao baada ya beki wake, Masoud Nassoro 'Chollo' kukosa penati sekunde chache kabla ya filimbi ya mwisho.
Simba ambayo ilipata ushindi mfululizo tangu ilipotoka kwenye Kombe la Mapinduzi ambapo walinyakua kwa kuifunga kwa mikwaju ya penati Mtibwa Sugar, walianza kupata bao kupitia kwa Ibrahim Hajibu aliyefunga kwa mkwaju wa adhabu ndogo nje kidogo ya lango la Mbeya City dakika chache kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili katika pambano hilo lililochezwa wenye uwanja wa Taifa, Mbeya walionyesha upinzani mkali zaidi na kufanikiwa kurejesha bao katika dakika ya 77 kupitia Hamad Kibopile kabla ya kupata penati katika muda wa ziada kupitia kwa Yusuph Abdalla baada ya kipa wa Simba Peter Manyika Jr kucheza faulo.
Hata hivyo mfungaji wa bao hilo alifanya kosa la kizembe la kumchezea vibaya Jonas Mkude na kupewa penati ambayo Chollo aliipoteza na pambano hilo kumalizika kwa Simba kulala kwa mabao 2-1.
Kipigo hicho kimewafanya baadhi ya wanachama kjuucharukia uongozi wa juu wa klabu hiyo sambamba na Kamati ya Mashindano wakidai wameshindwa kufanya kazi.
Kwa ushindi huo wa leo Mbeya ambayo ilienda mapumziko Novemba 9 wakiwa mkiani mwa msimamo wa ligi hiyo, imechupa toka nafasi ya 13 hadi nafasi ya 7 wakiwa na pointi 15 na Simba kusaliwa na pointi  13 na kushuka hadi nafasi yua 11.
Simba itashuka dimbani tena Jumamosi kukabiliana na JKT Ruvu ambao wapo katika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 18 sawa na Yanga.

No comments:

Post a Comment