STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 28, 2015

Ommy Dimpoz akiri kutengeneza video na Avril si mchezo!

Dimpoz akiwa na Avril
Avril
Dimpoz na Avril
MSANII nyota nchini, Omar Nyembo 'Ommy Dimpoz' amesema haikuwa kazi rahisi kwake kutengeneza video na mwanadada Judith Mwangi 'Avril' aliyeimba naye wimbo uitwao 'Hello Baby'.
Dimpoz aliyeshirikishwa katika wimbo huo ambao 'audio' na video yake zinafanya vema hewani Afrika Mashariki kati zilipoachiwa, alinukuliwa na mtandao wa Bongo5 kwamba utengenezaji wa video ya wimbo huo ulikuwa mtihani mgumu kwake.
Msanii huyo alisema Avril ni mrembo ambaye jicho la mwanamme yeyote rijali ni vigumu kuvumilia anapobadilisha nguo mbele yake ili kuinogesha video, lakini yeye alijikaza kiume.
'Ilikuwa mtihani kidogo unajua kufanya kazi na msichana mrembo ushawishi unakuwa mwingi. Kwa hiyo nilikuwa najizuiazuia," alisema kabla ya kuongeza;
"Kwa sababu kwenye video kuna mambo mengi, mtu anaweza akatokea akabadilisha nguo mbele yako, kwa hiyo yote niliyavumilia, ni lazima uvumilie majaribu ili kazi iende," alinukuliwa mkali huyo.
Dimpoz alidokeza pia namna picha zake na Arvil katika utengenezaji video alizotupia kwenye mtandao wa Instagram zilivyotaka kuibua kasheshe kwa mchumba wa mwanadada huyo mrembo

No comments:

Post a Comment