STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 3, 2015

Chelsea nouma, yafanya kufuru usajili dirisha dogo

http://cdn.caughtoffside.com/wp-content/uploads/2015/02/Chelsea-Juan-Cuadrado.jpg
Kifaa kipya kilichotua Chelsea
DIRISHA dogo la usajili nchini Uingereza limefungwa usiku wa jana huku klabu ya Chelsea ikiwa ndiyo timu inayoongoza kwa kutumia fungu kubwa la fedha katika usajili huo kwa kumchukua winga wa kimataifa wa Colombia Juan Cuadrado kwa kitita cha paundi milioni 23.3.
Kwa ujumla klabu za Ligi Kuu zimetumia kiasi cha paundi milioni 130 katika usajili huu hivyo kufikia kiwango kama walichotumia mwaka jana.
Klabu ya Crystal Palace ndio iliyokuwa na harakati nyingi katika siku ya mwisho ya usajili kwa kuwachukua wachezaji wanne akiwemo Wilfried Zaha.
Klabu ya Hull City ndio iliyofunga dirisha hilo kwa kutangaza usajili wa kumchukua mshambuliaji wa Lokomotiv Moscow Dame N’Doye katika muda wa mwisho.
Jumla ya wachezaji 13 wamesajiliwa katika siku ya mwisho ya usajili huku 35 zaidi wakisajiliwa katika kipindi chote toka dirisha lilipofunguliwa Januari mosi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment