STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 3, 2015

Kocha Redknapp abwaga manyanga QPR

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2012/11/24/1353767357535/Harry-Redknapp-new-QPR-ma-008.jpg
Kocha Harry Redknapp aliyebwaga manyanga QPR
KOCHA wa timu ya Ligi Kuu ya England ya  Queen Park Rangers, Harry Redknapp ametangaza kujiuzulu kuwa kocha wa timu hiyo.
Redknapp huyo  mwenye umri wa miaka 67 amedumu na klabu hiyo kwa takribani miaka miwili ameamua kuachana na klabu hiyo kwa hiari yake baada ya kushindwa kuopa mafanikio.
Taarifa kutoka kwa Tony Fernandes inasomeka hivi; "Tunashukuru kwa kila alichofanya Redknapp hapa klabuni wakati wote wa utawala wake kama kocha."
Taarifa hiyo ya kujiuzulu kwa kocha huyo haijaeleza wazi chanzo cha kujiuzulu kwa kocha huyo ambaye pia aliwahi kuifundisha Tottenham Hotspurs na kuipa mafanikio akisi cha kupigiwa debe kuchukua mikoba ya kuifundisha timu ya taifa ya England.
Hata hivyo inaelezwa tatizo la kiafya alilonalo kocha huyo ndilo lililomfanya achukue uamuzi huo wa kutekma kibarua hicho.
Redknapp amekunuliwa akisema kuwa maumivu ya magoti yanayomsumbua kwa muda mrefu kiasi cha kuweza kusimama kwa muda mrefu ndicho sababu ya kuacha kibarua hicho na kumpigia simu bosi wake Tony Fernandes ili atafute mtu wa kuisimamia timu hiyo iliyopo nafasi ya pili mkiani mwa msimamo wa Ligi.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

No comments:

Post a Comment