STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 3, 2015

Viporo FA: Manchester Utd kutoka vipi leo?! Liverpool kesho

http://mufclatest.com/wp-content/uploads/2015/02/Cambridge-United-FA-Cup-Replay-750x360.png
http://i3.mirror.co.uk/incoming/article5032437.ece/alternates/s615/Cambridge-United-v-Manchester-United-FA-Cup-Fourth-Round.jpg
Man United walivyohenyaka mechi ya kwanza kwa Cambridge United, leo watatokaje
BAADA ya kushukizwa ugenini kwa kulazimishwa suluhu isiyo na magoli dhidi ya timu ya daraja la pili ya Cambridge United, leo watakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford kurudiana na timu hiyo katika mechi ya Raundi ya Nne ya Kombe la FA.
Katika michuano ya kombe hilo, leo kutakuwa na mechi nyingine mbili zitakazowakutanisha timu za Fulham  na Sunderland ambazo zilishindwa kutambiana katika mechi yao ya kwanza kwa kutoka sare ya 0-0, huku timu zilizofungana bao 1-1 katika mechi iliyopita Sheffield United na  Preston North End nao wataonyeshana kazi.
Bolton Wanderers waliowasimamisha Livepool nyumbani kwao Anfield watakuwa wenyeji wa Liverpool katika mechi nyingine itakaypogwa kesho kukamilisha mechi za viporo vya michuano hiyo kabla ya kuanza mechi za raundi ya tano.
Manchester Utd ambayo imetoka kupata ushindi mnono wa mabao 3-1 nyumbani katika Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya vibonde wa ligi hiyo Leicester City italazimika kugangamala ili wasije wakaenda na maji kama ilivyowakuta timu za Manchester City na Chelsea waliotolewa nishai na timu za madaraja ya chini katika michuano hiyo.
Kocha Luis Van Gaal anatarajiwa kuchezesha kikosi kamili katika pambano hilo ili kuweza kuvuka hatua hiyo na kujiweka katika nafssi nzuri ya kunyakua angalau kombe moja kati ya mawili ambayo wana nafasi ya kuyatwaa wakigangamala lingine likiwa la Ligi Kuu japo ana nafasi finyu.
Mabingwa hao wa zamani na wenye historia kubwa katika FA kwa kunyakua mara nyingi, imeshaondoshwa kwenye Kombe la Ligi (Capital One) na pia haishiriki michuano yoyote ya kikmataifa baada ya msimu uliopita kuwa na wakati mgumu chini ya kocha David Moyes.

No comments:

Post a Comment