STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 3, 2015

Hatem Ben Arfa kustaafu soka mapema?!

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/benarfa_2.jpg
Hatem Ben Arfa anayedaiwa huenda akastaafu?
WAKILI wa Hatem Ben Arfa amedokeza kiungo huyo anaweza kustaafu soka baada ya Ligi ya Soka ya Ufaransa-LFP kumfungia kucheza mechi za mashindano na klabu ya Nice.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 27 alijiunga na Nice akitokea Newcastle United mapema mwezi huu baada ya mkopo wake katika klabu ya Hull City kusitishwa.
Kwa mujibu wa taratibu za Shirikisho la Soa Dunia-FIFA, wacheza wanaweza kuruhusiwa kucheza mechi za mashindano katika vilabu viwili pekee kwa msimu.
Wakili Jean-Jacques Bertrand amesema ni wazi kuwa uwepo wa Ben Arfa katika timu hiyo utamalizika leo na kuhofu kuwa mchezaji huyo anaweza kuwa anafikiria kustaafu.
Ben Arfa aliifungiwa Newcastle katika ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Readings kwa timu za vijana chini ya umri wa miaka 25 Agosti mwaka jana kabla ya kwenda Hull kwa mkopo ambako nako alicheza mechi tisa.

No comments:

Post a Comment